ZIJUE ATHARI ZA MADINI YA URANI


TANZANIA ni moja ya nchi zilizojaliwa kuwa na rasilimali nyingi zinazopatikana katika maeneo mbalimbali, rasilimali hizo ni pamoja na madini ya aina mbalimbali kama vile almasi, dhahabu, tanzanite, makaa ya mawe, mekyuli na Urani.

Maana ya Urani

Urani ni madini, kwa kitaalamu hufahamika kama uranium na ni ya kemikali katika kundi la metali ambapo hutoa mionzi inayoweza kubadilika kwa haraka na kusababisha athari kubwa kama tahadhari haikuchukuliwa.
Madini haya hupatikana ardhini, kwenye mawe na kwa kiasi kidogo kwenye maji, kwa Tanzania baadhi ya kampuni kama vile Mantra (T) Ltd na Uranex (T) Limited zimefanya utafiti katika maeneo ya Namtumbo (Mkuju River Project), Bahi na Manyoni na kugundua uwepo wa Madini hayo.

Matumizi ya Urani

1.    Urani hutumika kuzalisha nguvu za nyuklia (nuclear energy) ambazo husaidia  kuzalishwa kwa Umeme wa uhakika.
2.    Urani hutumika kutengenezea silaha mfano: risasi (bullets) na mabomu.
3.    Uzani atomia 238 ya Urani hutumiwa na wanasayansi kubashiri umri wa miamba iliyodumu kwa miaka mingi.

Athari za Urani kwenye Mazingira

1.    Uchimbaji wa Urani huitaji eneo kubwa la ardhi hivyo misitu mingi hukatwa na kuharibiwa, viumbe vingi  vinavyotegemea misitu (bioanuwai) huweza kuharibiwa na kupotea kabisa.
2.    Pale patakapochimbwa madini hayo hutokea uchafuzi vyanzo ya Maji (mfano: Mito, Visima na Chemichemi) na hii inatokana na matumizi ya kemikali kama vile zebaki na tindikali za salfa ambazo hutumika katika hatua mbalimbali za uchimbaji wa Urani.

3.    Uchimbaji wa Urani husababisha migogoro ya ardhi kwa kuwaondoa au kuwahamisha watu (wafugaji au wakulima) katika maeneo yao ya Makazi ili kupisha Shughuli za uchimbaji.

Athari za Urani Kiafya

Madini ya urani yanaweza kuingia kwa mwanadamu kwa njia tofauti ikiwemo kuvuta vumbi liliopo kwenye hewa au kumeza kwa njia ya chakula,maji au kupenya kwenye mwili (ngozi) kwa kupitia mionzi yake na kusababisha madhara Kiafya kama ifuatavyo:

1.    Urani ni sumu inayoathiri mwili kwa kusababisha saratani ya figo, ubongo, ini na damu.

2.    Urani husababisha magonjwa ya Moyo, watoto kufia tumboni, kupungua kwa kinga ya mwili, vifo vya watoto, kuharibika kwa mimba, watoto kuzaliwa na uzito mdogo, kuathiriwa kwa chembechembe za uzazi za urithi na watoto kuzaliwa na ulemavu wa ubongo.

Jinsi ya kukabiliana na Athari za Urani

1.    Tathmini ya Athari za mazingira lazima ifanywe mapema kabla, wakati na baada ya kuanza kwa shughuli za uchimbaji ili kuandaa njia sahihi za kujikinga na Athari zitakazojitokeza.
2.    Wachimbaji na wananchi wanaoishi jirani na maeneo ya uchimbaji ni muhimu waelimishwe jinsi ya kukabiliana na athari za Urani.

  
Soma zaidi HAPA

1 comment:

  1. This is over-exaggerated! There is rarely epidemiological evidence to support some highlighted claims. If there are no sufficient scientifically proven evidence to some claims then we use the "Precautionary principle". This is how scientific blaming are based! Yet, there is a plan truth that Uranium is weakly radioactive and heavy metal.Therefore, its chemical toxicity supersede the radiological component!As a heavy metals accumulated in Kidney and Heart...Its biological half life is significant..so can damage.....That's all Kunda...Goodluck

    ReplyDelete