Ulimwengu hauishi
maajabu, vituko na vijambo. je waweza kuamini kwamba burger ya kwanza
kutengenezwa maabara kwa kutumia seli za ng’ombe imepikwa na kuliwa katika
mkutano wa habari jijini London!?
Habari zilizoifikia ‘AFYA
YA MAZINGIRA’ zinasema kwamba burger hii ilitengenezwa maabara kwa kutumia seli
kutoka kwa mnyama aina ya Ng’ombe ambapo seli hizo zilioteshwa maabara hadi
zikawa nyama (muscles) kisha nyama hiyo ikatumika kutengeneza chakula
kinachopendwa na wengi aina ya burger.
Ubunifu huu wa
kutengeneza nyama kwa kutumia seli za ng’ombe unakuja miezi michache tangu
shirika la chakula na kilimo duniani (FAO) kutangaza kwamba baada ya miaka kadhaa
watu watalazimika kula wadudu kutokana na uhaba wa chakula unaoelekea kuikumba
dunia kutokana na ongezeko kubwa la watu (high population) na uhaba wa mvua
unaotokana na mabadiliko ya hali ya hewa (climatic change).
Wanasayansi waliobuni
teknolojia hiyo wanasema “teknolojia hii itasaidia sana kutokana na kuongezeka
kwa watu wengi duniani wanaohitaji vyakula vinavyotokana na nyama”.
Mmoja wa watu
waliofanikisha kuionja nyama hiyo ni mtafiti wa chakula wa Austraria, Bw.
Ruetzler ambapo baada ya kuionja alisema “nilidhania kwamba nyama hii ingekuwa
laini sana…ina radha nzuri inayofanana na nyama lakini haina majimaji kama
nyama ya kawaida”.
“Ufanano uko sahihi kabisa japo kuwa nimekosaa
chumvi na pilipili”. Bw. Ruetzler alitania.
Akiongea na vyombo vya
habari, kiongozi wa utafiti uliogundua teknolojia hiyo mpya, prof. Mark Post
kutoka chuo kikuu cha Maastricht amesema nyama hiyo imetengenezwa kwa kutumia
idadi ya mabilioni ya seli zilizo kuzwa maabara, na kuongeza kwamba itachukua
muda kidogo hadi pale nyama hizo zitakapoanza kusambazwa masokoni.
WE ARE FACING PROBLEM OF GETTING THESE
ReplyDeleteIMPORTANT STUFFS ....WE NEED TO BE PUBLIC SO THAT MANY PEOPLE CAN GET THEM EASY .
EVERYTHING THAT WE DO LET THEM BE ACESIBLE SO THAT EVERYBODY CAN GET WHAT WE ARE IMPORTANT TO A WHOLE SOCIETY .LET US BE COMMITED TO
SAVE LIFE
SERVE PEROPLE
AND SERVE OURSELVES THEN