Ni wiki moja tu imepita
tangu Serikali iifunge machinjio ya Ukonga Mazizini kutokana na kuendesha shughuli
zake kwenye hali ya uchafu, mabucha yaliyokuwa Ukonga mazizini yamehamishiwa
karibu na machinjio ya vingunguti na kupelekea hali ya mazingira ya uchafu
maeneo hayo.
Msimamizi wa machinjio
ya Vingunguti, Dk. Juma Nganyagi amethibitisha kutokea kwa hali hilo na kusema
kwamba uongozi unalifanyia kazi suala hilo.
Machinjio ya Ukonga
mazizini ilifungwa na waziri wa nchi, ofisi ya makamu wa rais (mazingira), Dk.
Terezya Huvisa kwa kuendesha shughuli zake katika mazingira ya uchafu na kuhatarisha
Afya za walaji wa nyamba.
Uchunguzi uliofanywa na
vyombo vya habari umeonesha kwamba watu wengi waliokuwa wanafanyia shughuli zao
kwenye machinjio ya Ukonga Mazizini wamehamia machinjio ya Vingunguti na
kuongeza idadi ya ng’ombe wanaochinjwa machinjioni hapo zaidi ya mara mbili. Kwasasa
miundombinu ya machinjio hiyo imezidiwa na ongezeko kubwa la wanyama
wanaochinjwa na wanaosubiri kuchinjwa.
Pia uchunguzi huo
umebaini kwamba hali ya usafi na afya maeneo hayo imekuwa mbaya sana kwakuwa
waendeshaji wa shughuli za uchinjaji machinjioni hapo hawafuati sheria za Afya
na Mazingira.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA
No comments:
Post a Comment