MABADILIKO YA HALI YA HEWA YAKARIBISHA MILIPUKO WA MAGONJWA MENGINE



Mabadiliko ya hali ya hewa yamekuwa yakielezwa kusababisha mabadiliko ya ghafla ya majira, kuyeyuka kwa barafu na kupanda kwa kina cha bahari. Lakini tumesahau madhara makubwa ya kuenea kwa magonjwa ambayo yanaweza kutokea kwa binadamu, mimea na wanyama.

Kuongezeka kwa joto kuna badilisha mazingira yetu kwa kuondoa ulinzi wa asili dhidi ya magongwa na hivyo kuvifanya vimelea vya magonjwa kuishi maisha marefu yenye mafanikio tele.

Dalili kubwa tunaweza kuziona kwenye maeneo ya baridi ya pembezoni mwa dunia (North Pole), ambapo imeripotiwa kuongezeka kwa minyoo (parasitic worms) inayoathiri wanyama wa huko (musk ox na reindeer) na athari hizo zinaonekana kusambaa kwa kasi maeneo mengine.

Ukanda wa joto kama vile visiwa vya Caribbean umeripotiwa kuongezeka kwa joto linaloathiri mahusiano ya viumbe vya majini (symbiosis) na kuvifanya viumbe hivyo viwepo hatarini kupata magonjwa. Pamoja na kuwepo na athari kwenye mahusiano hayo lakini pia imeripotiwa kuwepo kwa ongezeko la ukuaji wa bacteria hatari kwenye ukanda huo.

Katika nchi zinazoendelea (ikiwemo Tanzania) kumekuwapo na ongezeko la vimelea (pathogens) ambavyo vimekuwa vikiathiri kilimo na viumbe mwitu (wildlife) na hivyo kuhatarisha usalama wa chakula na maisha ya watu waishio maeneo hayo.

USHAURI: Ili kujikinga na magonjwa ya binadamu yanayoweza kuchochewa na mabadiliko ya hali ya hewa, serikali inapaswa kuwaongezea nguvu wadau wa afya wanaojishughulisha na ufuatiliaji wa magonjwa (disease surveillance), udhibiti wa wadudu waenezao vimelea vya magonjwa (vector control), usafi wa mazingira (waste management and sanitation), Madawa (Drugs), Chanjo (Vaccines), Usalama wa Chakula (food safety and security) na shughuli zingine za KINGA.



No comments:

Post a Comment