UTAFITI: VINYWAJI VYA SUKARI HUSABABISHA UTAPIAMLO KWA WATOTO



Utafiti uliofanyika kwenye mji wa Charlottesville nchini marekani umebaini kwamba watoto walio na umri wa chini miaka mitano wanaokunywa vinywaji vya sukari kila siku wako hatarini kuwa na uzito uliopitiliza (utapiamlo) ukilinganisha na wale wanaokunywa vinywaji hivyo mara chache au kutokunywa kabisa.

Dk. mark de Bour wa chuo kikuu cha Virginia ambae alioongoza utafiti huo alisema yeye pamoja na watafiti wenzake walifanya utafiti kwa wazazi wa watoto 9,500 waliozaliwa mwaka 2001 ambapo umri wa watoto waliofanyiwa utafiti ulikuwa ni miaka miwili, mine na mitano. Utafiti huo ulizingatia kiwango cha uchumi na elimu cha wazazi na muda ambao watoto hao hupewa vinywaji vya sukari na kuangalia luninga. Watoto pamoja na wazazi wao walipimwa uzito wakati utafiti ulipokuwa ikiendelea.

Utafiti huo uligungua kwamba uwiano (propotional) wa watoto wanaokunywa japo soda moja kwa siku na vinywaji vingine vya sukari ulikuwa ni kati ya 9% hadi 13% kutegemea na umri wao.

baada ya utafiti huo watafiti walibainisha kuwa watoto wenye umri wa miaka mitano wanaokadiliwa  kunywa angalau soda moja kwa siku walikuwa ni sawa na asilimia 43%, walikuwa hatarini zaidi  ya kupata utapiamlo ukilinganisha na watoto wanaokunywa vinywaji vya sukari mara chache au kutotumia kabisa.

Na watoto wa miaka minne ambao wameripotiwa kunywa vinywaji vya sukari kwa wastani walionekana kuwa wengi wao wana uzito uliopitilza kuliko watoto wasiotumia.
 
Utafiti huo haukuonesha uhusianao kati ya matumizi ya vinywaji vyenye sukari na kuzidi kwa uzito kwa watoto walio chini ya miaka miwili. Hali iliyohitimisha kuwa matumizi ya vinywaji vya sukari kwa watoto chini ya miaka mitano yanaleta utapiamlo kwa kadri muda wa matumizi ya vinywaji hivyo unavyoongezeka.



Kusoma zaidi BOFYA HAPA



No comments:

Post a Comment