Vyombo vya habari
nchini china vimeripoti kutokea kwa kifo cha mtu mwingine kilichotokana na aina
mpya ya ugonjwa wa mafua ya ndege ambapo mpaka sasa idadi ya vifo kwa ugonjwa
huo imefikia watu 44.
Habari za kuaminika
kutoka nchini humo zinasema mtu huyo mwenye umri wa miaka 61 kutoka jimbo la
kaskazini mwa china, hebei, amefariki dunia siku ya jumatatu (jana) kutokana na
viongo vya ndani kushindwa kufanya kazi (multiple organ failure), kabla ya kufa
mtu huyo alipimwa mnamo tarehe 20 mwezi wa 7 na kugundulika ana virusi vya
ugonjwa huo (H7N9 virus).
Mpaka sasa idadi yawatu
walioripotiwa kuambukizwa ugonjwa huo nchini china imefikia 134.
Ugonjwa huu mpya wa
mafua ya ndege (H7N9) ulioikumba China
inasemekana kuwa ni hatari na unaoua kwa haraka zaidi ukilinganisha na ugonjwa
wa mafua ya ndege unaoenezwa na virusi vya H5N1ambao umeua zaidi ya watu 360
ndani ya kipindi cha miaka kumi iliyopita. Imesemekana kirusi hiki kipya (H7N9)
kinaweza kujibadilisha (mutate) and kupata uwezo wa kusambaa kiurahisi.
Mwanzoni mwa mwezi huu
wanasayansi walitoa ripoti ya kesi (case) ya kwanza ya uwezekano wa kusambaa (probable
case) kwa kirusi hiki cha H7N9 kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine tofauti
na mwanzo ambapo ilifikiriwa kwamba kirusi hiki kina uwezo wa kutoka kwa ndege
peke yake kwenda kwa binadamu.
Source: VOA
No comments:
Post a Comment