‘ARSENIC’ YABAINIKA KULETA MADHARA ZAIDI KWA BINADAMU


Arsenic ni elementi ya sumu inayopatikana ardhini na majini ikiungana sulfa au metali zingine. 

Kwa muda mrefu Arsenic imekuwa ikijulikana kusababisha madhara kwa binadamu, madhara hayo ni saratani, magonjwa ya moyo, na magonjwa ya ufahamu. Utafiti mpya wa hivi karibuni umebaini kwamba kunywa maji yenye kiasi kidogo sana cha elementi ya Arsenic kunaweza kuharibu mapafu, na kuongeza kwamba madhara yanaweza kuwa makubwa zaidi iwapo itaingia kwa mtu anaevuta sigara.


Utafiti huo ulikuwa ni sehemu ya mradi wa muda mrefu ambao ulifanywa Bangladesh inchini India, ambapo takribani nusu ya watu wapatao milioni 77 wanaishi kwenye maeneo yenye visima vya maji (groundwater wells) vilivyosheheni kiwango kikubwa cha elementi za arsenic.

Kwa muda wa zaidi ya miaka mitano, watafiti walikuwa wakijaribu kupima uwezo wa mapafu kwa wagonjwa 950 ambao walihudhuria kwenye vituo vya afya kwa matatizo ya mfumo wa hewa (upumuaji). Vipimo vya wagonjwa hao vililinganishwa na kiasi cha arsenic kilichokutwa ndani ya miili yao. Matokeo yalionyesha kwamba athari za arsenic kwenye mapafu zinatofautiana kulingana na kiasi cha arsenic (Dose) kilichoingia kwa mgonjwa, matokeo hayo yalichapishwa  kwenye jarida la America Journal of Respiratory and Critical Care Medicine.

Watu waliokunywa maji yenye kiwango nusu ya kile kinachokubaliwa kimataifa hawakuonyesha dalili zozote za madhara ya mapafu, wale waliokunywa maji yenye kiasi cha arsenic mara 10 ya kile kilichoruhusiwa walionyesha dalili za kushindwa kupumua vyema (Loss of breathing function), wale waliokunywa maji yenye arsenic zaidi ya mara kumi (10>) ya kiwango kilichoruhusiwa walionyesha dalili mbaya zaidi za kushindwa kupumua sawasawa na mtu aliyevuta tumbaku kwa miongo (decades) mingi na kuwafanya wawe hatarini kupata magonjwa hatari ya njia ya hewa (serious respiratory diseases).

Kujua kiwango cha arsenic kilichoruhusiwa kwenye maji ya kunywa Tanzania BOFYA HAPA


No comments:

Post a Comment